Monday 11 February 2008

Tanzania Bila Rushwa Na Ufisadi Inawezekana


Kila kona ya mitaa ya Bongo utakuta bango kubwa lenye ujumbe kama linavyoonekana kwenye picha, hapo juu...ningependa kuona mabango kama hayo yenye ujumbe usemao TANZANIA BILA RUSHWA NA UFISADI INAWEZEKANA TUWEKE MIFUMO WAZI....Nimefurahi kuona wabunge wote wameungana kupigania maslahi ya wananchi badala ya kutetea maslahi ya wachache wenye tamaa zisizokuwa na mipaka katika kujikusanyia mali kwa njia zisizo halali hivyo kuhatarisha uchumi wa nchi. Muda wa kulindana umekwisha, muda wa UKADA umekwisha sasa tushirikiane wote waliopewa madaraka na wasiokuwa na madaraka, tubadili misimamo yetu kwa maslahi ya nchi kwa ujumla. ningependa kuona Rais katika baraza jipya kuna waziri japo mmoja toka katika kambi ya "UPINZANI" ili kutoa ishara kuwa michango yao katika bunge inalenga kutetea maslahi ya taifa na wananchi wake kwa ujumla, tuondokane na siasa za chuki za kuona hata kama mpinzani akileta hoja yenye kutetea wananchi basi chama tawala lazima kipinge kwa nguvu zote. Huu ni muda wa kushirikiana wote tulete maendeleo ya nchi kwa haraka..Tumechoka kuitwa nchi masikini wakati UTAJIRI wetu unachukulia hivi hivi tungali macho tena wengine tunasaidia kubeba kupeleka nje ya nchi huku wananchi wanaishi kwenye mabanda ya mabati mabovu yaliyofunikwa kwa maplastiki...

hakuna ajira vijana wamebaki kuwa wakabaji na majambazi...madada nao wamekuwa wakijiuza kwenye kwenye kona za jiji...

2 comments:

Anonymous said...

oya activate blog mara kwa mara

Anonymous said...

Hello. This post is likeable, and your blog is very interesting, congratulations :-). I will add in my blogroll =). If possible gives a last there on my blog, it is about the Perfume, I hope you enjoy. The address is http://perfumes-brasil.blogspot.com. A hug.